Tarehe Iliyotumwa 2022-09-28 17:39:35
Utoaji wa mafunzo ya uandishi wa Ramani ya Kitabu (Book map)
Watendaji wa Taasisi ya Elimu ya Zanzibar wametakiwa kuhakikisha wanafuatilia kwa makini Mafunzo wanayopewa juu ya uandishi wa vitabu ili watoto wapate vitabu vyenye ubora. Ameyasema hayo Kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Mkuu wa divisheni ya utayarishaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia Bi Mchanga Ame Saleh ,kutoka Taasisi ya Elimu ya Zanzibar, wakati akifungua Mafunzo juu ya namna ya utayarishaji wa Ramani ya Kitabu ( book map) kwa Watendaji wa Taasisi hiyo katika ukumbi wa kituo Cha Elimu Mbadala Raha Leo mjini unguja, amesema Mafunzo hayo ni muhimu sana kwaajili ya kuwa jengea uwezo watendaji wa Tasisi ya Elimu katika utayarishaji wa vitabu vya kiada pamoja na miongozo ya walimu. Aidha amesema Mafunzo yame kuja wakati muwafaka wakati Taasisi ipo katika hatua ya uandishi wa vitabu vitakavyo tumika katika Mtaala unaotarajiwa kutumika mwakani January 2023. Amesema kupitia Mafunzo haya watendaji wataweza kuandaa vitabu vya watoto vilivyo Bora vitakavyo saidia kujenga msingi na kuimarisha uwezo wa kusoma, kuhesabu na kuandika . Aidha ame sisitiza kuwa kutumia fursa hii kwa makini juu ya taaluma inayo tolewa kwaajili ya Taifa letu. Nae Bwana Masumbuko Ephrahim, Ambae ni mshauri wa kuandaa vitabu vya Elimu kutoka kampuni ya Exford Dar es salaam, amesema lengo ni kuwawezesha watendaji wa Tasisi ya Elimu ya Zanzibar kuweza kuchambua mihutasari na kuandaa mpango wa uandishi wa vitabu vya Maandalizi na Msingi Zanzibar. Amefahamisha kuwa ili kitabu kiweze kukidhi malengo ya jumla na yale mahususi yalio ainishwa kwenye sera ya Elimu na kwenye mihutasari ya masomo husika ni lazima kuzingatia umahiri na ubunifu ili kipatikane kitabu Bora. Nao washiriki wa Mafunzo hayo wameishukuru Taasisi ya Elimu ya Zanzibar kwa kuweza kuwapatia Mafunzo ya namna ya utayarishaji wa vitabu kwaajili ya Taifa letu.
Tarehe Iliyotumwa 2022-07-22 10:20:41
Taasisi ya Elimu ya Zanzibar inaendelea kuhamasisha uwepo wa mabadiliko ya mtaala kwa kuimarisha vifaa vya kufundishia ikiwemo Miongozo ya ufundishaji Ili Walimu Wafundishe kwa umahiri zaidi.
Taasisi ya Elimu ya Zanzibar inaendelea kuhamasisha uwepo wa mabadiliko ya mtaala kwa kuimarisha vifaa vya kufundishia ikiwemo Miongozo ya ufundishaji Ili Walimu Wafundishe kwa umahiri zaidi. Akifungua Warsha ya uimarishaji wa Miongozo ya kufundishia Makamo Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri kutokaTaasisi ya Elimu ya Zanzibar Ndugu Salma Haji Saadat kwa maafisa wa baraza la mtihani, waratibu wa vituo vya walimu, washauri wa masomo, wakaguzi, wahadhiri wa vyuo vikuu, wakufunzi wa vyuo vya ualimu vya serikali na binafsi na walimu kutoka skuli za serikali na binafsi katika kituo Cha walimu cha Michakaini Wilaya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba. Amesema Mabadiliko yoyote yakitokea lazima yaendane na mabadiliko ya Walimu kwani wao ndio wanaolengwa kwaajili ya kufundisha Wanafunzi. Amesema Mtaala wa Elimu ya Maandalizi na Msingi unatatarajiwa kuwa suluhisho ya kuwa na Elimu bora na utaondosha Malalamiko mengi ya Wadau kuona kuwa watoto wanasoma masomo mengi. Hivyo uwepo wao hapa kwa sababu wao ni Wakaguzi pia wataenda kutoa Ushauri katika kulenga Yale masuala Tunayotarajia kupata. Aidha amewashauri washiriki wawe huru katika kuchangia kwaajili ya kutengeneza Elimu kwani wameaminiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutengeneza Elimu Bora. Nae Mratibu wa Taasisi ya Elimu Pemba Bi Asha soud Nassor ,ame sema waitumie fursa hii kutumia Taaluma zao ili kuweza kufanikisha kazi hiyo na kufikia lengo lililo kusudiwa kwaajili ya Taifa letu. Washiriki wa Warsha hiyo wamesema kazi hii ni kazi ya kitaifa kwani wanaenda kutengeneza mustakbali wa Elimu kwa watoto wetu. Wamesema Hili ni jambo jema kwani limewashirikisha Wadau wengi wa Elimu kwa ajili ya kutoa maoni yetu. Aidha Tunaishukuru Taasisi ya Elimu Zanzibar kwa kushirikisha katika kazi hiyo kwani wanacho kifanya ni kwaajili ya Taifa letu. Hata hivyo wame washukuru wawezeshaji wa Warsha hiyo kwa kuwapa muongozo mzuri katika kufanya kazi hii kwani umahiri wao umewapa uwelewa wa kufanya kazi kwa ufanisi. Warsha hii inafanyika kwa Wadau tofauti Unguja na Pemba.
Tarehe Iliyotumwa 2023-02-07 12:45:34
Utoaji wa mafunzo kwa wataalamu kwa wasarifishaji wa vitabu
Taasisi ya Elimu ya Zanzibar imesema inaendelea na juhudi zake kuhakikisha Taifa linanapata Mtaala bora pamoja na vifaa vyakufundishia hususan vitabu. Akifungua Mafunzo ya usarifishaji wa vitabu vinavyotumika katika Skuli za Serikali na Binafsi za Unguja na Pemba Meneja wa Rasilimali Watu,Utawala na Mipango, Taasisi ya Elimu ya Zanzibar Ndugu Mussa Hassan zyuma katika ukumbi wa kituo Cha walimu kiembe samaki. Amesema Taasisi ya Elimu kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar baada ya kutayarisha mitaala huendelea na hatua ya kutayarisha vitabu na vifaa vyengine vya kufundishia. Amesema kwa sasa Taasisi ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha mapitio ya Mtaala mpya kwa ngazi ya Maandalizi na Msingi ili uweze kutumika ifikapo mwaka 2023. Aidha amesema kukamilika kwa Mtaala huo unaenda sambamba na vifaa vya kufundishia ikiwemo vitabu vya Wanafunzi na Walimu. HivyoTaasisi ya Elimu ya Zanzibar, Imeeandaa Mafunzo haya kwa lengo la kupata Wataalamu wao wa ndani ili waweze kutayarisha vitabu na vifaa Bora vya kufundishia. Nae Mkufunzi wa mafunzo hayo Ndugu Haji Khamis Mdungi Ambae ni Mkuu wa Seksheni ya kusarifu Machapisho kutokaTaasisi ya Wakala wa Serikali uchapaji Zanzibar Amesema Taasisi ya Elimu kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Imeeandaa mafunzo hayo kwa lengo la kuhakikisha ushiriki wa kila mtu unapatikana . Kwa upande wao Washiriki wa mafunzo hayo wamesema Mafunzo hayo yatawasaidia sana kujua namna ya usafirishaji wa vitabu nchini. Mafunzo hayo ya siku kumi yame wahusisha Maafisa kutoka Wizara ya Elimu Zanzibar pamoja na Taasisi ya Elimu ya Zanzibar.