Taasisi ya Elimu ya Zanzibar inaendelea na warsha ya kuandaa mpango wa mafunzo ya utekelezaji wa Mtaala mpya wa vyuo vya ualimu kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu Zanzibar. Warsha hiyo imehusisha walimu wastaafu wa chuo cha ualimu Nkrumah, wahadhiri kutoka chuo kikuu cha Taifa cha Zanzibar na Maafisa wengine wa WEMA chini ya muwezeshaji kutoka Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM).
Taasisi ya Elimu ya Zanzibar ni Wakala wa Serikali chini ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar iliyoanzishwa mwaka 2011 kwa kuzingatia matakwa ya Sera ya Elimu ya mwaka 2006. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeona kuna umuhimu wa kuwa na chombo cha kuratibu na kusimamia mitaala na utafiti wa elimu ili kuimarisha ubora wa elimu hapa Zanzibar. Kwa mujibu wa Sheria Namba 4 ya mwaka 2016 iliyoanzisha Taasisi ya Elimu ya Zanzibar, Taasisi ina mamlaka ya kutayarisha mitaala, vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa skuli za Maandalizi, Msingi, Sekondari, Vyuo vya Ualimu na Elimu isiyorasmi na Watu wazima. Aidha Taasisi inajukumu la kufanya tafiti za kielimu na kutoa mafunzo juu ya utekelezaji wa mitaala.
Kiongozi wa kuandaa mitaala bora na sahihi kutokana na utafiti kwa matumizi ya skuli na vyuo vya ualimu Zanzibar.
Kuongoza utaratibu wa kuandaa mitaala na vifaa bora vya kufundishia na kujifunzia kwa lengo la kuwa na elimu bora na sahihi kupitia utafifiti na ushirikishwaji wa wadau ili kukidhi matakwa ya watu wa Zanzibar
Huduma zinazotolewa na Taasisi ya Elimu ya Zanzibar.
Kuishauri Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar juu ya mambo yanayohusiana na ukuzaji Mitaala ya Elimu ya Maandalizi, Msingi, Elimu ya Sekondari pamoja na Vyuo vya Ualimu
Kufanya tafiti za Elimu na Kuthibiti Ubora kwenye vifaa vya kufundishia na kujifunzia
Kuratibu Utayarishaji wa Vifaa vya Kufundishia na Kujifunzia kwa walimu na wanafunzi
Kutoa Mafunzo kazini yanayohusiana na Mitaala na Vifaa vya Kufundishia na Kujifunzia