- Mkutano wa mwaka wa Jukwaa la Viongozi wa Elimu ya Sekondari
- Mafunzo ya Mfumo wa Masjala (e-office)
- Uzinduzi wa programu 10 za Redio za kujifunza lugha ya Kiingereza
- Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu
- Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu - Pemba
- Utiaji saini Mkataba wa Uchapishaji Vitabu kwaajili ya Skuli binafsi Zanzibar
- Kikao cha kutathmini utekelezaji wa Mradi wa Elimu Mjumuisho Zanzibar
- Mafunzo ya Utekelezaji wa Mtaala mpya kwa Walimu wa Maandalizi na Msingi wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu ya kielimu.
- Mafunzo ya Mtaala mpya kwa Walimu wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu
- Kikao kazi cha Kubadilishana Uzoefu katika Masuala ya Elimu ya Watu Wazima
- Ziara ya Kujenga Uhusiano mwema
- Mjumbe wa Sekretarieti ya GPE Lucinda Ramos ametembelea TEZ
- Mahafali ya Skuli ya High Achievement
- TEZ yapokea Ugeni kutoka Gambia
- TEZ yafanya Mkutano na Walimu wakuu wa Skuli za Sekondari Pemba
- TEZ na TET kuandaa muongozo wa kutolea mafunzo ya utekelezaji wa Mtaala mpya kwa walimu wa Sekondari.
- UDOM na TEZ kukusanya maoni ili kutengeza Moduli mpya za mafunzo ya walimu wa Msingi na Sekondari.
- WEMA Kupokea Ripoti ya upembuzi yakinifu (needs assessement report) ya Upitiaji wa Mitaala ya Mafunzo ya Ualimu.
- Mafunzo ya Mtaala mpya kwa walimu wa Skuli za Sekondari Zanzibar
- Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri ngazi ya Sekondari yameanza Kisiwani Pemba.
- Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri kwa Wakufunzi ambao wanatarajiwa kuwafundisha walimu wanaofundisha elimu ya msingi (darasa la tatu)
- Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri kwa Wakufunzi.
- Warsha ya kuandaa Mfumo wa upimaji wa ' Large Scale Assessment'
- Ufungaji wa Warsha ya Siku tano ya kuandaa Mfumo wa upimaji wa \' Large Scale Assessment\'.
- Mkutano na wadau kukusanya maoni juu ya Mkakati wa Mawasiliano Kuhusu Mtaala wa Umahiri “Curriculum Communication Strategy”.
- Mafunzo ya Mtaala wa Umahiri kwa Waajiriwa wapya wa kada ya ualimu wa ngazi ya (Maandalizi na Msingi).
- Meneja wa ZIE afungua kikao kazi cha Watendaji Shirika la Room to read.
- Kikao baina ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar na Taasisi ya Goethe Institute ya Ujerumani

Uzinduzi wa Mafunzo kwa Walimu - Mtaala Mpya
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Ali Abbdulgulam Hussein amesema kuna umuhimu mkubwa wa kutoa elimu kwa jamii juu ya Mtaala Mpya wa elimu, ili waweze kuutambuwa vizuri. Ameeleza hayo alipokuwa akifunguwa mafunzo ya mtaala mpya kwa waalimu wa Maandalizi na Msingi, yaliyoandaliwa na Taasisi ya Elimu Zanzibar, yaliyofanyika Kituo cha walimu (TC Dunga), wilaya ya Kati Unguja. Amesema kuwa mtaala huo mpya wa umahiri utawajenga watoto kusoma kwa kudadisi na kuelewa haraka mambo jambo amnalo ni tofauti na hapo zamani ambapo walikuwa wakisoma kwa nadharia. “Mafunzo haya muyape umuhimu kuliko chochote na mutowe mafunzo mazuri kwa watoto ili wawe na mafananikio mazuri na pia muwe mabalozi wazuri kuhusiana na mtaala huu ambao kutokana na upya wake utakuwa na changamoto”, alisema. Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Elimu Zanzibar Nd. Abdalla Mohamed Mussa amesema uwepo wa mtaala huo mpya wa ujenzi wa umahiri kutaleta mabadiliko katika sekta ya elimu. Aidha amesema mafunzo ni ya awamu ya pili ambapo katika awamu ya kwanza walitoa mafunzo kwa walimu 6,557 wa maandalizi na msingi kwa skuli za serikali na binafsi na awamu hii ya pili watatoa kwa walimu 6,457 kwa skuli zote za Zanzibar.