Taasisi ya Elimu ya Zanzibar inaendelea na warsha ya kuandaa mpango wa mafunzo ya utekelezaji wa Mtaala mpya wa vyuo vya ualimu

Taasisi ya Elimu ya Zanzibar inaendelea na warsha ya kuandaa mpango wa mafunzo ya utekelezaji wa Mtaala mpya wa vyuo vya ualimu kwa wakufunzi wa vyuo vya ualimu Zanzibar. Warsha hiyo imehusisha walimu wastaafu wa chuo cha ualimu Nkrumah, wahadhiri kutoka chuo kikuu cha Taifa cha Zanzibar na Maafisa wengine wa WEMA chini ya muwezeshaji kutoka Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM).