- Mkutano wa mwaka wa Jukwaa la Viongozi wa Elimu ya Sekondari
- Mafunzo ya Mfumo wa Masjala (e-office)
- Uzinduzi wa programu 10 za Redio za kujifunza lugha ya Kiingereza
- Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu
- Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu - Pemba
- Utiaji saini Mkataba wa Uchapishaji Vitabu kwaajili ya Skuli binafsi Zanzibar
- Kikao cha kutathmini utekelezaji wa Mradi wa Elimu Mjumuisho Zanzibar
- Mafunzo ya Utekelezaji wa Mtaala mpya kwa Walimu wa Maandalizi na Msingi wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu ya kielimu.
- Mafunzo ya Mtaala mpya kwa Walimu wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu
- Kikao kazi cha Kubadilishana Uzoefu katika Masuala ya Elimu ya Watu Wazima
- Ziara ya Kujenga Uhusiano mwema
- Mjumbe wa Sekretarieti ya GPE Lucinda Ramos ametembelea TEZ
- Mahafali ya Skuli ya High Achievement
- TEZ yapokea Ugeni kutoka Gambia
- UDOM na TEZ kukusanya maoni ili kutengeza Moduli mpya za mafunzo ya walimu wa Msingi na Sekondari.
- WEMA Kupokea Ripoti ya upembuzi yakinifu (needs assessement report) ya Upitiaji wa Mitaala ya Mafunzo ya Ualimu.
- Mafunzo ya Mtaala mpya kwa walimu wa Skuli za Sekondari Zanzibar
- Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri ngazi ya Sekondari yameanza Kisiwani Pemba.
- Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri kwa Wakufunzi ambao wanatarajiwa kuwafundisha walimu wanaofundisha elimu ya msingi (darasa la tatu)
- Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri kwa Wakufunzi.
- Warsha ya kuandaa Mfumo wa upimaji wa ' Large Scale Assessment'
- Ufungaji wa Warsha ya Siku tano ya kuandaa Mfumo wa upimaji wa \' Large Scale Assessment\'.
- Mkutano na wadau kukusanya maoni juu ya Mkakati wa Mawasiliano Kuhusu Mtaala wa Umahiri “Curriculum Communication Strategy”.
- Mafunzo ya Mtaala wa Umahiri kwa Waajiriwa wapya wa kada ya ualimu wa ngazi ya (Maandalizi na Msingi).
- Meneja wa ZIE afungua kikao kazi cha Watendaji Shirika la Room to read.
- Kikao baina ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar na Taasisi ya Goethe Institute ya Ujerumani
.jpeg)
TEZ yafanya Mkutano na Walimu wakuu wa Skuli za Sekondari Pemba
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Elimu ya Zanzibar Nd. Abdalla M. Mussa amewataka walimu wakuu wa skuli za Sekondari kisiwani Pemba kujiandaa na mapokezi ya Mtaala mpya wa Sekondari ambao utaanza kutumika hivi karibuni kwa Skuli zote nchini. Akizungumza katika Mkutano maalumu na walimu wakuu wa Skuli za sekondari Mkoa wa Kaskazini na Kusini Pemba huko katika Kituo cha Walimu Mitiulaya na Skuli ya Sekondari Madungu Amesema, Taasisi ya Elimu ya Zanzibar imeshaanza kuandaa Mchakato wa kutoa Mafunzo kwa Walimu wa skuli za Sekondari ambayo yatahusisha walimu wote wa skuli za serikali na binafsi. Amesema Mtaala mpya wa sekondari utawawezesha wanafunzi kujitegemea na kuweza kujiajiri wanapomaliza masomo ambapo mfumo wa Elimu ya Sekondari utakuwa na mikondo miwili ambayo ni Mkondo wa Amali na Mkondo wa Masomo ya kawaida. Ameelza kuwa katika mtaala huo kutakuwa na masomo mapya ambayo ni Pamoja na somo la Historia ya Tanzania na somo la Business study. Sambamba na hayo amewasisitiza walimu kutoa ushirikiano kwa kuhakikisha wanatoa Takwimu sahihi za Walimu wanaohitaji kupatiwa mafunzo ili kila Mwalimu apate fursa ya Mafunzo hayo. Nao walimu wakuu wa skuli za sekondari Wameishukuru Taasisi ya Elimu ya Zanzibar kwa kuwapatia Tarifa muhimu kuhusu mtaala mpya kila inapohitajika na kushauri kupatiwa Mihutasari na vitabu kwa wakati.