- Mkutano wa mwaka wa Jukwaa la Viongozi wa Elimu ya Sekondari
- Mafunzo ya Mfumo wa Masjala (e-office)
- Uzinduzi wa programu 10 za Redio za kujifunza lugha ya Kiingereza
- Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu - Pemba
- Utiaji saini Mkataba wa Uchapishaji Vitabu kwaajili ya Skuli binafsi Zanzibar
- Kikao cha kutathmini utekelezaji wa Mradi wa Elimu Mjumuisho Zanzibar
- Mafunzo ya Utekelezaji wa Mtaala mpya kwa Walimu wa Maandalizi na Msingi wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu ya kielimu.
- Mafunzo ya Mtaala mpya kwa Walimu wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu
- Kikao kazi cha Kubadilishana Uzoefu katika Masuala ya Elimu ya Watu Wazima
- Ziara ya Kujenga Uhusiano mwema
- Mjumbe wa Sekretarieti ya GPE Lucinda Ramos ametembelea TEZ
- Mahafali ya Skuli ya High Achievement
- TEZ yapokea Ugeni kutoka Gambia
- TEZ yafanya Mkutano na Walimu wakuu wa Skuli za Sekondari Pemba
- TEZ na TET kuandaa muongozo wa kutolea mafunzo ya utekelezaji wa Mtaala mpya kwa walimu wa Sekondari.
- UDOM na TEZ kukusanya maoni ili kutengeza Moduli mpya za mafunzo ya walimu wa Msingi na Sekondari.
- WEMA Kupokea Ripoti ya upembuzi yakinifu (needs assessement report) ya Upitiaji wa Mitaala ya Mafunzo ya Ualimu.
- Mafunzo ya Mtaala mpya kwa walimu wa Skuli za Sekondari Zanzibar
- Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri ngazi ya Sekondari yameanza Kisiwani Pemba.
- Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri kwa Wakufunzi ambao wanatarajiwa kuwafundisha walimu wanaofundisha elimu ya msingi (darasa la tatu)
- Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri kwa Wakufunzi.
- Warsha ya kuandaa Mfumo wa upimaji wa ' Large Scale Assessment'
- Ufungaji wa Warsha ya Siku tano ya kuandaa Mfumo wa upimaji wa \' Large Scale Assessment\'.
- Mkutano na wadau kukusanya maoni juu ya Mkakati wa Mawasiliano Kuhusu Mtaala wa Umahiri “Curriculum Communication Strategy”.
- Mafunzo ya Mtaala wa Umahiri kwa Waajiriwa wapya wa kada ya ualimu wa ngazi ya (Maandalizi na Msingi).
- Meneja wa ZIE afungua kikao kazi cha Watendaji Shirika la Room to read.
- Kikao baina ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar na Taasisi ya Goethe Institute ya Ujerumani

Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Elimu Zanzibar Nd.Abdalla Mohamed Mussa amewataka Walimu wa Skuli za Maandalizi kuacha tabia ya kufanya kazi kimazowea na badala yake kutumia mbinu sahihi za kufundishia ikiwemo kuwashirikisha wanafunzi. Ameyasema hayo wakati akitoa nasaha kwa walimu wa maandalizi wanao patiwa mafunzo ya mtaala mpya yanayoendela katika kituo cha Walimu Wingwi na Mitiulaya Mkoa wa Kaskazini Pemba, amesema ni vyema walimu kutumia vitabu vya ziada na kiada kama nyenzo za kufundishia na sio kutumia vitabu vya Wanafunzi pekee. Aidha ameeleza kuwa mafunzo ya Mtaala mpya yatawasaidia kufahamu mbinu bora za utekelezaji wa mtaala huo na kuchochea mabadiliko kupitia ubunifu na vitendo kama mtaala unavyohitaji. Kwa upande wake Mkuu wa divisheni ya Mafunzo kwa Walimu kutoka Taasisi ya Elimu ya Zanzibar Bi.Mwana Ali Abdallah amesema Serikali imetumia gharama kubwa kuwekeza katika ya sekta ya elimu hivyo amewataka walimu kuyapokea Mafunzo hayo na kuyafanyia kazi. Akitao neno la shukurani Mratibu wa kituo cha Walimu Wingwi Nd, Abdallah Muhammed Shehe ameipongeza Wizara ya Elimu kupitia Taasisi ya Elimu kwa Kuratibu mafunzo hayo na kuahidi kuyafanyia kazi kwa Lengo la kuimarisha mafanikio katika Sekta ya Elimu Nchini.