- Mkutano wa mwaka wa Jukwaa la Viongozi wa Elimu ya Sekondari
- Mafunzo ya Mfumo wa Masjala (e-office)
- Uzinduzi wa programu 10 za Redio za kujifunza lugha ya Kiingereza
- Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu
- Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu - Pemba
- Utiaji saini Mkataba wa Uchapishaji Vitabu kwaajili ya Skuli binafsi Zanzibar
- Kikao cha kutathmini utekelezaji wa Mradi wa Elimu Mjumuisho Zanzibar
- Mafunzo ya Utekelezaji wa Mtaala mpya kwa Walimu wa Maandalizi na Msingi wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu ya kielimu.
- Mafunzo ya Mtaala mpya kwa Walimu wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu
- Mjumbe wa Sekretarieti ya GPE Lucinda Ramos ametembelea TEZ
- Mahafali ya Skuli ya High Achievement
- TEZ yapokea Ugeni kutoka Gambia
- TEZ yafanya Mkutano na Walimu wakuu wa Skuli za Sekondari Pemba
- TEZ na TET kuandaa muongozo wa kutolea mafunzo ya utekelezaji wa Mtaala mpya kwa walimu wa Sekondari.
- UDOM na TEZ kukusanya maoni ili kutengeza Moduli mpya za mafunzo ya walimu wa Msingi na Sekondari.
- WEMA Kupokea Ripoti ya upembuzi yakinifu (needs assessement report) ya Upitiaji wa Mitaala ya Mafunzo ya Ualimu.

Kikao kazi cha Kubadilishana Uzoefu katika Masuala ya Elimu ya Watu Wazima
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Elimu ya Zanzibar Abdalla Mohamed Mussa akiwa na Maafisa Taasisi hiyo wamekutana na Uongozi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) Dar-es-salaaam. Lengo la kukutana Taasisi hizo ni kujifunza kwa kubadilishana Uzoefu katika Masuala ya Elimu ya Watu Wazima na kujenga Uhusiano Mwema baina ya TEZ na TEWW Tanzania Bara. Mkutano huo umeongozwa na Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu wazima Prof. Michael Ng\'umbi. Mapema Maafisa wa Taasisi ya Elimu ya Zanzibar walifanya ziara katika Vituo mbalimbali vya Elimu ya Watu Wazima ambavyo ni Pamoja na Kituo cha Elimu ya Watu wazima Morogoro (WAMO) kinachofundisha watoto wa kike ambao walipata matatizo mbalimbali na kukaisha masomo, kituo cha CLC Ruvu JKT (MUKEJA) na vituo vya IPOSA-Temeke na Bahati Dar-es-salaam.