- Mkutano wa mwaka wa Jukwaa la Viongozi wa Elimu ya Sekondari
- Mafunzo ya Mfumo wa Masjala (e-office)
- Uzinduzi wa programu 10 za Redio za kujifunza lugha ya Kiingereza
- Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu
- Utiaji saini Mkataba wa Uchapishaji Vitabu kwaajili ya Skuli binafsi Zanzibar
- Kikao cha kutathmini utekelezaji wa Mradi wa Elimu Mjumuisho Zanzibar
- Mafunzo ya Utekelezaji wa Mtaala mpya kwa Walimu wa Maandalizi na Msingi wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu ya kielimu.
- Mafunzo ya Mtaala mpya kwa Walimu wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu
- Kikao kazi cha Kubadilishana Uzoefu katika Masuala ya Elimu ya Watu Wazima
- Ziara ya Kujenga Uhusiano mwema
- Mjumbe wa Sekretarieti ya GPE Lucinda Ramos ametembelea TEZ
- Mahafali ya Skuli ya High Achievement
- TEZ yapokea Ugeni kutoka Gambia
- TEZ yafanya Mkutano na Walimu wakuu wa Skuli za Sekondari Pemba
- TEZ na TET kuandaa muongozo wa kutolea mafunzo ya utekelezaji wa Mtaala mpya kwa walimu wa Sekondari.
- UDOM na TEZ kukusanya maoni ili kutengeza Moduli mpya za mafunzo ya walimu wa Msingi na Sekondari.
- WEMA Kupokea Ripoti ya upembuzi yakinifu (needs assessement report) ya Upitiaji wa Mitaala ya Mafunzo ya Ualimu.
- Mafunzo ya Mtaala mpya kwa walimu wa Skuli za Sekondari Zanzibar
- Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri ngazi ya Sekondari yameanza Kisiwani Pemba.
- Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri kwa Wakufunzi ambao wanatarajiwa kuwafundisha walimu wanaofundisha elimu ya msingi (darasa la tatu)
- Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri kwa Wakufunzi.
- Warsha ya kuandaa Mfumo wa upimaji wa ' Large Scale Assessment'
- Ufungaji wa Warsha ya Siku tano ya kuandaa Mfumo wa upimaji wa \' Large Scale Assessment\'.
- Mkutano na wadau kukusanya maoni juu ya Mkakati wa Mawasiliano Kuhusu Mtaala wa Umahiri “Curriculum Communication Strategy”.
- Mafunzo ya Mtaala wa Umahiri kwa Waajiriwa wapya wa kada ya ualimu wa ngazi ya (Maandalizi na Msingi).
- Meneja wa ZIE afungua kikao kazi cha Watendaji Shirika la Room to read.
- Kikao baina ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar na Taasisi ya Goethe Institute ya Ujerumani

Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu - Pemba
Taasisi ya Elimu Zanzibar imesema itaendelea kutoa mafunzo ya mara kwa mara kwa Walimu wa maandalizi na msingi juu ya mtaala mpya wa umahiri ili kuwajengea uwezo Walimu katika ufundishaji wao. Akifunga mafunzo ya siku 5 ya Mtaala wa umahiri kwa walimu wa maandalizi mwaka wa pili wa Mkoa wa Kusini Pemba huko kituo cha Walimu Michakaini Kisiwani Pemba, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Elimu ya Zanzibar Abdalla Mohamed Mussa amesema kufuatia mabadiliko ya mtaala Taasisi ya Elimu inalazimika kutoa Mafunzo kwa walimu na kuwapatia vifaa vya kufundishia ikiwemo vitabu. Amesema serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar inaendelea kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya Elimu, hivyo ni vyema walimu wakaendana na mageuzi hayo ili waweze kutekeleza kazi zao kwa weledi na kutengeneza Taifa lenye wasomi. Mapema Mratibu wa Taasisi ya Elimu Zanzibar Kisiwani Pemba Bi Asha Soud Nassor amesema walimu wameonyesha maendeleo mazuri katika muda wa mafunzo hayo ya siku tano hivyo jamii itegemee mabadiliko makubwa kwa wanafunzi wa skuli za Serikali na binafsi. Wakizungumzia mafunzo hayo baadhi ya waalimu wameipongeza Taasisi ya Elimu ya Zanzibar kwa kusimamia vyema Mafunzo hayo na kuahidi kuwa mabalozi wazuri kwa walimu wengine Zaidi ya walimu Elfu Sita wanaendelea kupatiwa Mafunzo hayo wakiwemo wa skuli za Serikali na za Binafsi kwa wilaya zote za Unguja na Pemba.