- Mkutano wa mwaka wa Jukwaa la Viongozi wa Elimu ya Sekondari
- Mafunzo ya Mfumo wa Masjala (e-office)
- Uzinduzi wa programu 10 za Redio za kujifunza lugha ya Kiingereza
- Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu
- Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu - Pemba
- Utiaji saini Mkataba wa Uchapishaji Vitabu kwaajili ya Skuli binafsi Zanzibar
- Kikao cha kutathmini utekelezaji wa Mradi wa Elimu Mjumuisho Zanzibar
- Mafunzo ya Utekelezaji wa Mtaala mpya kwa Walimu wa Maandalizi na Msingi wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu ya kielimu.
- Mafunzo ya Mtaala mpya kwa Walimu wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu
- Kikao kazi cha Kubadilishana Uzoefu katika Masuala ya Elimu ya Watu Wazima
- Ziara ya Kujenga Uhusiano mwema
- Mjumbe wa Sekretarieti ya GPE Lucinda Ramos ametembelea TEZ
- Mahafali ya Skuli ya High Achievement
- TEZ yapokea Ugeni kutoka Gambia
- TEZ yafanya Mkutano na Walimu wakuu wa Skuli za Sekondari Pemba
- TEZ na TET kuandaa muongozo wa kutolea mafunzo ya utekelezaji wa Mtaala mpya kwa walimu wa Sekondari.
- UDOM na TEZ kukusanya maoni ili kutengeza Moduli mpya za mafunzo ya walimu wa Msingi na Sekondari.

WEMA Kupokea Ripoti ya upembuzi yakinifu (needs assessement report) ya Upitiaji wa Mitaala ya Mafunzo ya Ualimu.
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imepokea ripoti ya upembuzi yakinifu (needs assessement report) ya Upitiaji wa Mitaala ya Mafunzo ya Ualimu. Ripoti hiyo imewasilishwa na Taasisi ya Elimu ya Zanzibar kwa kushirikiana na Washauri Elekezi kutoka vyuo vikuu vya Tanzania (UDOM, UDSM na SUZA) kwa kushirikiana na wataalamu wa ndani. Ripoti hiyo itaisaidia Wizara katika utekelezaji wa Mtaala wa Vyuo vya ualimu kwa kuzingatia urejeshwaji wa chuo cha Nkrumah ambapo ubora wa mitaala ni jambo muhimu katika kuimarisha chuo na kupata walimu bora nchini. Kikao hicho kimeongozwa na Naibu Katibu Mkuu Taaluma Dkt. Mwanakhamis Adam Ameir ambapo wadau wa Elimu wakiwemo viongozi wa Wizara, Taasisi zisizo za kiserikali (NGOs) na Taasisi mbalimbali za kieleimu walitoa maoni yao ili kuboresha uandaaji wa Mtaala wa Vyuo vya ualimu.